Thursday 27 November 2008

JE, UKIMWI NI MAAMBUKIZO SAWA NA MALARIA?

Ni kitu gani cha kwanza watu hufikilia endapo utawaambia kwamba una maambukizo ya ukimwi?, ndio, moja kwa moja watasema "huyu alikuwa malaya kabla ya kuambukizwa", au "Ameyataka mwenyewe, kulala lala ovyo" na mengineyo mengi ambayo hayamsaidii huyo aliyeathirika na ukimwi bali humvunja nguvu na kumpotezea hata yale mategemeo madogo aliyokuwa nayo. Je, hii ni kwa sababu ukimwi hauna dawa ya kuponya kabisa ugonjwa huu?. Je, dawa ya ukimwi ikipatikana watu watasema nini juu ya waathirika wa ugonjwa huu?. Ndio, ukimwi utakuwa ni ugonjwa wenye dawa kama vile gonorrhea(http://www.emedicinehealth.com/gonorrhea/article_em.htm), cifillis, chlamydia na mengineyo yanayoambukizwa kwa kujamiiana.

Kujamiiana ni mahitaji ya kimwili na mimi binafsi sioni kama ni tatizo kwa watu wazima wawili wenye akili timamu kufanya tendo hilo, ikiwa tuu, wote wawili kila mmoja pekee hana uhusiano huo na mtu mwingine. Kama haiwezekani ni vizuri mtu huyo atumie condoms kwani ni njia salama zaidi ya kuepuka maambukizo ya magonjwa ya zinaa.

Mipira hii ikitumiwa vizuri haitoboki kirahisi, kutoboka kwa mipira hii mara nyingi hutokana na kufungua na kisu, kiwembe, kalamu ya risasi au meno. Pia kuna sababu nyingine nyingi angalia kwenye site http://www.embarrassingproblems.co.uk/condoms_b.htm. Jingine ni kwamba unaweza kuwa na ukimwi na kutomuambukiza mpenzi wako kama mna jamiiana salama.

Jitihada za kutafuta dawa ya ukimwi zinaonekana na mda si mrefu tatizo hili litafumbuliwa, pengine kuna watu hawajui kuhusu PEP, ambayo husimama badala ya "Post Exposure Treatment" Hii ni dawa ambayo inaweza kuzuia maambukizo ya virusi vya ukimwi kwenye cell za binadamu baada ya kujamiiana na mtu mwenye ukimwi (http://www.aids.org/factSheets/156-Treatment-After-Exposure-to-HIV-PEP.html). Inasemekana kwamba wadudu wa ukimwi huchukua siku tatu kuanza safari yao ndani ya mwili baada ya kuingia kwenye semen. Hivyo dawa hii inawazuia kuianza ile safari na ndio maana dawa hii haiwezi fanya kazi kama utaitumia masaa 72 baada ya kujamiiana. Wanashauri kutumia dawa hii upesi iwezekanavyo, kwamba hii dawa iko more effective (kumradhi kwa kutumia lugha ya watu) kama ikitumiwa mapema. Dawa zingine za ukimwi zinazotumika sasa ni kama NRTIs, NNRTIs, Protease Inhibitors, Fusion Inhibitors na HAART.

Jamani, ukimwi ni ugonjwa wa maambukizo kama malaria ama influenza (flu)?. Ukimwi unaweza kunipata mimi, wewe na yule, tunatakiwa tuwe makini wakati wa kujamiiana tutumie mipira na pia tuwe na mpenzi mmoja tuu.

Wana jamii tunaomba maoni yenu juu ya mada hii, kama una mjadala kuhusu ukimwi tutumie, kama wewe umeambukizwa na unahitaji msaada wa kifikra unakaribishwa.