Monday 1 December 2008

JE UNAJUA UNAWEZA KUTOMUAMBUKIZA MTOTO UKIMWI AKIWA TUMBONI

Mpaka sasa watu wengi wanajua kwamba inawezekana kuzuia kumuambukiza mtoto ukimwi toka kwa mama wakati angali bado tumboni. Lakini je ni wajawazito wangapi Tanzania walioathirika na ukimwi wana uwezo huo wa kununua dawa ili kukinga watoto wao wasiambukizwe?. Matokeo yake kadili ya watoto 500,000 wana maambukizo ya ukimwi kila mwaka. Blog hii ya ukimwi na mimi leo hii, siku ya ukimwi duniani inahamasisha jamii yetu, kuiomba serikali yetu ya Tanzania kuangalia jinsi ya kusaidia wakina mama wajawazito na kuimarisha PMTCT (Preventing Mother To Child Transmission).

Maambukizo haya kwa mtoto yanaweza kutokea katika kipindi cha mimba, uchungu, kuzaa ama wakati wa kunyonyesha. Bila matibabu kadilia ya asilimia 30% ya watoto huzaliwa na maambukizo katika kipindi cha mimba au kuzaa, na karibu asilimia 20 ya watoto huambukizwa kwa njia ya kunyonyesha.

Tafadhali bonyeza kwenye hii link ina maelezo mengi mazuri yanaweza kusaidia: http://www.avert.org/motherchild.htm.

No comments: